Shirikisho la serikali za wanafunzi wa elimu ya juu Tanzania (TAHLISO) limetoa muda wa wiki moja kwa wanafunzi waliokosa mikopo licha ya kuwa na vigezo vyote ikiwemo uhitaji kusikilizwa na serikali kabla hatua nyingine hazijachukuliwa.
Tamko hilo limetolewa Leo na Mwenyekiti wa shirikisho hilo Bwana Stanslaus Peter, katika kikao cha pamoja kilichohusisha marais was vyuo vyote nchini, waliokutana jijini Dar es salaam Leo, kujadili sintofahamu inayowakumba wanafunzi wanaojiunga mwaka wa kwanza katika vyuo mbalimbali nchini.
Stanslaus amesema kuwa kuna kundi kubwa la wanafunzi ambao wameondolewa kwenye orodha ya wanufaika, na wengine kunyimwa kabisa ama kwa visingizio au bila sababu, jambo linalowafanya waishi katika mazingira magumu na kuhatarisha hatma yao kimasomo.
Amesema wamekubaliana kuwa, endapo serikali haitafanya kazi ombi hilo ndani ya wiki moja, basi shirikishi hilo litachukua hatua ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wanafunzi was mwaka wa pili na watatu kuungana na wale wa mwaka was kwanza katika kudai haki yao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
H. E SAMIA SULUHU HASSAN
Baada ya kifo cha aliyekuewa raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Hayari John Pombe Joseph Magufuli, aliekuwa makamu wake mama Samia S...
-
Habari kubwa kwenye vichwa vya magazeti ya Tanzania leo june 28, 2018, tukianza na Udaku , Michezo na Hardnews ...
-
Nyegere ni mnyama asiyeogopa chochote mile kwani anauwezo wa kuwakabili wanyama wakali na wakubwa kama simba au chui na wasimdhuru, ni mmoja...
-
Karibu tena, ni asubuhi nyingine tunakuleta habari mbalimbali za vichwa vya magazeti ya nyumbani Tanzania leo July 04, 2018, tukianza na...
No comments:
Post a Comment